Gari yako inatoa Maji kwenye Exhaust, Usipuuzie hali hii

Watu wengi sana wamekua wakijiuliza kitendo cha Gari kutoa maji kwenye Exhaust ina sababishwa na nini, na je ni tatizo katika gari yangu au ni kitu cha kutokuhofia. sasa soma nakala hii leo niweze kukujuza.

guides
11. Mar 2023
887 views
Gari yako inatoa Maji kwenye Exhaust, Usipuuzie hali hii

Katika hali ya kawaida, sio rahisi kuona maji yanayotoka kwenye mfumo wa Exhaust wa gari. Lakini ukigundua kuwa bomba lako la nyuma linavuja au linadondosha maji kutoka humo, basi ina maana kwamba mfumo wako wa kutolea moshi lazima uwe na maji ndani yake.

Hii sio sababu ya kuwa na wasiwasi sana kwa sababu kwa kawaida hali hii sio jambo kubwa. Hata hivyo, imekuwa ni jambo zuri kufanya uchunguzi wa hali hii na ukatenga muda kusoma nakala hii. Vinginevyo, inaweza kuunda matokeo mabaya zaidi ambayo yatakugharimu pesa nyingi kama usipojua tatizo nini.

zifuatazo ni baadhi ya sababu Kwanini Gari hutoa Maji kwenye Exhaust.

Kwanini Gari yangu inatoa maji kwenye Exhaust

1. Injini yako inafanya kazi vizuri

moja ya viashiria kua injini yako ipo vizuri hasa katika utendaji wake wa kazi ni kuona maji yanatoka kwenye Exhaust ingawa sio magari yote yanayotoa maji basi inaashiria hivi lakini magari mengi. Injini yako inapo unguza mafuta iwe petrol au diesel kinachofuata kama matokeo niĀ  Gas aina ya Kaboni dioksidi na maji. hii pia husaidia kupunguza kiwango cha hewa chafu kitakachotelewa na gari yako.

Pia sababu nyingine ya Gari kutoa maji kwenye Exhaust, kama unaishi kwenye maeneo yenye baridi kama Iringa, mbeya arusha na singida basi vitu kama hivi ni rahisi kuona kwani injini yako inapopata joto ile hewa ya baridi inayo ingia kwenye Exhaust. Kwa sababu hii, mvuke wa maji hutolewa wakati joto linapounganishwa na hewa baridi. Kisha utaona matone madogo ya maji yakianguka kutoka kwenye bomba la nyuma pamoja na kile kinachoonekana kuwa moshi mweupe. hata hivyo hali hii hutoweka baada ya muda mchache tu.

2. Piston yako ni mbovu

sababu nyingine ambayo husababisha maji kutoka kwenye mfumo wa kutolea hewa chafu yani Exhaust ni ubovu wa piston ya gari yako. lakini hii hua ina viashiria vyake kutambua kwamba kuna kitu hakipo sawa utaona vitu vifuatavyo.

Exhaust yako inatoa maji pamoja na moshi muda huo, ikiambatana na harufu isiyo ya kawaida, na maranyingi harufu hii hua ni nzuri na yenye kuvutia.

utakapo ona hali hii haraka sana usiendeshe gari yako na muite fundi wa mechanic aje akague piston yako kuthibitisha uwepo wa tatizo hilo.

Tuuzie Gari yako tembelea: magaribeipoa.com

Comments

No comments has been added on this post

Add new comment

You must be logged in to add new comment. Log in
Im Ibrahim a multifaceted individual with a passion for cars, SEO, and marketing. Ibrahim is an Expert in the Automotive sector.
Cars, Marketing, SEO
Categories
Toyota
Find all information including price, information and news about Toyota cars
guides
car guides
Updates
Resources
You will find downloadable resources in this category, Mostly PDFs
Questions
Get quick answers to all your questions
Lately commented
Thank you
UBOS Census recruitment 2024 U...
SO NICE
UBOS Census recruitment 2024 U...
I like the website so much
UBOS Census recruitment 2024 U...
Tanga mjini gharama ya kuvuta maji shingap
Gharama za kuvuta maji 2024 | ...
Are you a professional seller? Create an account
Non-logged user
Hello wave
Welcome! Sign in or register