Jinsi ya kupata leseni ya biashara online

Leseni Ya biashara inatolewa online kwasasa Tembelea mfumo wa Tausi tamisemi upate leseni kwa njia ya mtandao, pia unaweza fika katika ofisi za Halmashauri za Wilaya, Manispaa, Miji au Majiji na utapatiwa utaratibu.

Updates
1. Jul 2023
14411 views
Jinsi ya kupata leseni ya biashara online

Epuka usumbufu tembelea mfumo wa tausi tamisemi kupata leseni yako ya biashara yako kwa haraka.

Hakikisha kabla ya kuomba leseni ya biashara basi una TIN number, yani Utambulisho wa Mlipakodi na baada ya hapo mwombaji atatakiwa kuomba leseni ya biashara kutoka ofisi za Biashara katika Wilaya, Manispaa, Jiji na Wizara ya Biashara na Viwanda kwa kutegemea na aina ya biashara anayotaka kuanzisha. 

Aina za biashara watoaji wa leseni wamezigawa katika makundi mawili nayo ni  Kundi A na kundi B

Mfano wa Biashara zilizo kwenye Kundi B:

  • Wakala wa Bima
  • Vipuri (Spare parts)
  • Maduka ya dawa za Binadamu/Mifugo
  • Viwanda Vidogo 
  • Duka la rejareja na duka la jumla

Kwa biashara ya kundi A zinazo jumuisha viwanda vikubwa vinavyo ajiri watu wengi, mtaji mkubwa na pia hata eneo inalochukua inakua ni kubwa kiasi Leseni za Kundi A hutolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara.

soma pia:-

Jinsi ya kujaza leseni ya biashara

Kwanza uta Download fomu ya maombi ya leseni ya biashara, na baada ya hapo utajaza taarifa zako kama jina lako na utaambatanisha:-

  • Jina la Biashara kama sio mtu binafsi (Certificate of Incorporation or Registration).
  • “Memorandum and Article of Association” kama ni Kampuni
  • Kitambulisho cha mpiga kura, Cheti cha kuzaliwa au Hati ya kiapo kuonyesha kuwa ni Mtanzania na Mgeni Hati ya kuishi nchini daraja la “A” (Residnece Permit Class “A”).
  • Hati ya kiuwakili (Power of Attorney) kama wenye hisa wote wa Kampuni wapo nje ya nchi.
  • Ushahidi wa maandishi kuwa una mahali pa, kufanyia biashara (Kwa mfano hati za nyumba, mkataba wa upangishaji, risiti za malipo ya kodi za majengo au ardhi.
  • Hati ya kujiandikisha kama mlipa kodi TRA (TIN).

Kwa leseni zinazodhibitiwa na Mamlaka mbalimbali, Kwa mfano (TFDA, EWURA, TAURA, CRB, TILLI) n.k lazima mwombaji kuwa na leseni husika kabla ya kuomba leseni ya biashara fomu ya maombi ya biashara (TFN 211) hutolewa kwa ada ya Tshs. 1,000/=. 

NB: Leseni hii huisha muda wake mwaka mmoja (1) tangu tarehe ilipoanza kutumika.

Baada ya kujaza fomu na viambatanisho, maombi hupitishwa ngazi zinazotakiwa kisheria – Mpango Miji na Afya. Baada ya hapo leseni hutolewa ndani ya siku moja au mbili na si zaidi.

Faida za kua na leseni ya biashara

Kusajili biashara ina faida kadhaa muhimu. Hapa chini ni baadhi ya faida za kusajili biashara:

  1. Uhalali na Uaminifu: Kusajili biashara kunatoa hali ya uhalali na uaminifu kwa biashara yako. Inaonyesha kuwa biashara yako ni halali na imezingatia sheria na kanuni zinazohusiana na biashara hiyo.

  2. Ulinzi wa Jina la Biashara: Kusajili biashara kunakupa haki ya kipekee na ulinzi wa jina la biashara yako. Hii inamaanisha kuwa hakuna mtu mwingine anayeweza kutumia jina lile lile au jina linalofanana na biashara yako katika eneo la kijiografia lililosajiliwa.

  3. Kupata Mikopo na Uwekezaji: Benki na taasisi nyingine za fedha mara nyingi zinahitaji usajili wa biashara kabla ya kutoa mikopo au ufadhili. Kwa kuwa umesajili biashara yako, inakuwa rahisi kupata mikopo na uwekezaji kutoka vyanzo mbalimbali.

  4. Upatikanaji wa Soko: Kusajili biashara kunakupa fursa ya kufanya biashara na taasisi za umma, makampuni, au wateja wengine ambao wanahitaji ushahidi wa uhalali wa biashara unayofanya nao biashara.

  5. Ulinzi wa Mali na Dhima: Kusajili biashara kama kampuni inaweza kukupa ulinzi wa kibinafsi. Ikiwa biashara yako itashindwa au kukabiliwa na masuala ya kisheria, unaweza kuwa na kinga ya kibinafsi dhidi ya madeni ya biashara na hatari ya kupoteza mali yako binafsi.

  6. Ukuaji na Mafanikio: Kusajili biashara kunaweza kusaidia kujenga msingi imara wa ukuaji wa biashara. Inakupa fursa ya kushiriki katika zabuni za serikali, ushirikiano na makampuni mengine, na kuongeza sifa yako kama mtoa huduma au muuzaji.

Ni muhimu kukumbuka kuwa leseni ya biashara ni hati ya kuthibitisha uhalali wa kufanya biashara kisheria. Ni jukumu la mmiliki wa leseni kuhakikisha kuwa anafuata sheria na kufanya biashara kwa usalama wake na watumiaji wa bidhaa zake wakati wote.

 

 

Comments

No comments has been added on this post

Add new comment

You must be logged in to add new comment. Log in
Im Ibrahim a multifaceted individual with a passion for cars, SEO, and marketing. Ibrahim is an Expert in the Automotive sector.
Cars, Marketing, SEO
Categories
Toyota
Find all information including price, information and news about Toyota cars
guides
car guides
Updates
Resources
You will find downloadable resources in this category, Mostly PDFs
Questions
Get quick answers to all your questions
Lately commented
Thank you
UBOS Census recruitment 2024 U...
SO NICE
UBOS Census recruitment 2024 U...
I like the website so much
UBOS Census recruitment 2024 U...
Tanga mjini gharama ya kuvuta maji shingap
Gharama za kuvuta maji 2024 | ...
Are you a professional seller? Create an account
Non-logged user
Hello wave
Welcome! Sign in or register